
Mamlaka ya Urusi imethibitisha kuwa operesheni inaendelea katika Bahari Nyeusi, wakati ambapo wanajeshi wanajaribu kuinua kutoka chini mabaki ya ndege isiyo na rubani ya MQ-9 Reaper ya Marekani iliyoanguka siku moja kabla.
Maafisa wa utawala wa Marekani wanasema itakuwa vigumu sana kufanya hivyo na kusisitiza kuwa taarifa zote muhimu zilizomo kwenye ndege hiyo isiyo na rubani zimeharibiwa.
Hapo awali, Marekani ilisema ndege yake isiyo na rubani ya MQ-9 Reaper siku ya Jumanne iligongana na ndege ya kivita ya Urusi aina ya Su-27 ikiwa angani juu ya sehemu isiyo na vita upande wa Bahari Nyeusi na kuanguka majini.