fbpx

Mwanamitindo aonekana na nguo za mtanzania aliyepoteza begi 2018

Mbunifu wa mitindo wa Kitanzania asyakhamsin ambaye anaishi jijini Texas, Marekani, ameshangaa kuona mitindo yake, ambayo ilipotea pamoja na begi lake akiwa Uwanja wa Ndege wa Ronald Reagan Washington mnamo 2018, ikivaliwa na SamBrinton aliyekuwa naibu katibu msaidizi wa Matumizi ya Mafuta na Utupaji Taka katika Ofisi ya Nishati ya Nyuklia.

Khamsin alisema alipata picha za Brinton akiwa amevalia nguo zake za kitamaduni ambazo alikuwa amezipakia kwenye begi lililokosekana baada ya kujua kwamba Brinton alikuwa ameshtakiwa kwa kuiba vipande vingi vya mizigo kutoka kwa viwanja viwili vya ndege vya Marekani.

Mbunifu huyo wa mitindo alitweet picha zinazoonyesha baadhi ya nguo alizopoteza na picha za Brinton akiwa amevaa mavazi sawa.

“Niliona picha. Hiyo ilikuwa miundo yangu maalum, ambayo ilipotea kwenye begi hilo mnamo 2018, “aliiambia Fox News. “Alivaa nguo zangu, ambazo ziliibiwa.”

Begi la Khamsin lilitoweka kwenye Uwanja wa Ndege wa Ronald Reagan Washington mnamo Machi 9, 2018, baada ya kuruka hadi mji mkuu kwa hafla ambayo alipaswa kuweka nguo zake kwenye maonyesho, aliiambia Fox. Walakini, baada ya begi kutoweka hakuweza kushiriki.

Mumewe aliwasilisha ripoti kwa Idara ya Polisi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ya Metropolitan Washington na kuwasilisha madai kwa Shirika la Ndege la Delta, ambalo ni shirika la ndege ambalo Khamsin alitumia alivyosafiri kutoka Houston hadi DC. Begi halikupatikana tena.

Mawasiliano kati ya Delta na Khimson iliyoshirikiwa na Fox News yanaonyesha mwanamitindo huyo akiomba shirika la ndege limrudishie begi, akisema lilikuwa limejaa nguo za bei ghali, viatu, vito na vitu vingine vya kibinafsi.

Baada ya kuona picha za Brinton akiwa amevaa kile anachoamini kuwa ni nguo zake kwenye habari, aliwasilisha ripoti kwa Idara ya Polisi ya Houston mnamo Desemba 16. Mwishoni mwa Januari, alisema aliwasiliana na ofisi ya uwanja wa FBI huko Minneapolis, Minnesota.

“Polisi wa Houston, nadhani, [walituma] kesi hiyo kwa FBI huko Minnesota,” mume wa Khamsin aliiambia Fox. “Alipiga simu na kusema, ‘Niko [na] FBI, ninashughulikia kesi hii.’ Kisha mke wangu akampa taarifa na hatukusikia chochote. Hatujui kama kesi inaendelea. Hatujui kama kesi imepoa.”

FBI haikuthibitisha kuwa inachunguza, kulingana na sera ya shirika hilo. Kufikia Jumatano usiku, Brinton hakuwa ameshtakiwa kwa uhalifu wowote unaohusiana na nguo za Khamsin.

Brinton, 35, aliwahi kuwa naibu katibu msaidizi wa utawala wa Biden kwa matumizi ya mafuta na utupaji taka katika Ofisi ya DOE ya Nishati ya Nyuklia kabla ya kufukuzwa baada ya kushtakiwa kwa kuiba sanduku la mwanamke kutoka uwanja wa ndege wa Minneapolis mnamo Septemba na begi la mwanamke mwingine kutoka Uwanja wa ndege wa Las Vegas mwezi Julai.

Katika visa vyote vya Minnesota na Nevada, Brinton alikuwa amesafiri kwa ndege kutoka Washington, DC.,bna kuiba mabegi kwenye sehemu ya mizigo ya viwanja vya ndege, kulingana na malalamiko ya jinai yaliyopatikana na Fox News.

Brinton aliachiliwa bila dhamana na kuamriwa kutowasiliana na waathiriwa wowote wiki iliyopita baada ya kufikishwa mahakamani huko Minnesota.

Alifikishwa katika mahakama ya Las Vegas mwezi Disemba na kuachiliwa baada ya kutuma bondi ya $15,000. Hakimu, katika kesi hiyo, alimwambia afisa huyo wa zamani wa taka za nyuklia “kujiepusha na matatizo zaidi.”

Brinton anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela kwa wizi wa Minnesota na hadi miaka 10 jela kwa wizi wa Las Vegas, iwapo atakutwa na hatia.

Juhudi za kuwasiliana na Brinton na wakili wake huko Las Vegas hazikufaulu.

  • https://cast3.asurahosting.com/proxy/jambocom/stream

Verified by MonsterInsights